unfoldingWord 36 - Kubadilika Sura
Kontur: Matthew 17:1-9; Mark 9:2-8; Luke 9:28-36
Skript nömrəsi: 1236
Dil: Swahili
Tamaşaçılar: General
Məqsəd: Evangelism; Teaching
سمات: Bible Stories; Paraphrase Scripture
Vəziyyət: Approved
Skriptlər digər dillərə tərcümə və qeyd üçün əsas təlimatlardır. Onlar hər bir fərqli mədəniyyət və dil üçün başa düşülən və uyğun olması üçün lazım olduqda uyğunlaşdırılmalıdır. İstifadə olunan bəzi terminlər və anlayışlar daha çox izahat tələb edə bilər və ya hətta dəyişdirilə və ya tamamilə buraxıla bilər.
Skript Mətni
Siku moja, Yesu aliwachukua wanafunzi wake watatu Yakobo, Petro na Yohana. ( Mwanafunzi aitwae Yohana sio yule aliyembatiza Yesu.) Walipanda juu ya mlima mrefu kuomba pekeyao.
Yesu akiwa anaomba uso wake ulibadilika na kung'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama mwanga, yalikua meupe sana zaidi awezavyo mtu duniani kuyafanya yang'ae.
Ndipo Musa na nabii Eliya wakawatokea. Watu hawa waliishi duniani miaka mingi kabla. Waliongea na Yesu juu ya kifo chake ambacho kitatokea Yerusalemu siku chache baadae.
Wakati Musa na Eliya wanaongea na Yesu, Petro akamwambia Yesu, "Ni vizuri sisi kuwa hapa, hivyo naomba tutengeneze nyumba tatu moja ya kwako, nyingine ya Eliya na nyingine ya Musa". Lakini Petro hakujua alinenalo.
Wakati Petro anaongea wingu jeupe lilishuka na kuwazunguka na sauti ikatoka katika lile wingu ikisema " Huyu ni Mwanagu nimpendaye. Ninayependezwa naye msikilizeni yeye".Wale wanafunzi watatu waliogopa na kuanguka chini.
Ndipo Yesu akawagusa na kuwaambia "Msiogope inukeni". walipotazama pembeni ni Yesu pekee ndiye aliyebaki pale.
Yesu pamoja na wanafunzi wake watatu wakashuka kutoka mlimani. Yesu akawaambia "Msimwambie mtu yeyote yale yaliyotokea, siku chache baadae nitakufa kisha nitakua hai tena. Baada ya hapo mtawaambia watu."